
Siku imefika, tunafurahia
Tumejumuika, tunasherekea
Raha kwa hakika, imetuenea
Maarusi wetu, tunawapongeza
Leo ‘meungana, kwa njia halali
Muzidi pendana, mapenzi ya kweli
Hadi kwenye janna, muweni wawili
Maarusi wetu, tunawapongeza
Ndoa ni baraka, sunna ilo njema
Na haina shaka, ‘lioa hashima
Twaomba Rabuka, muishi daima
Maarusi wetu, tunawapongeza
Tupo furahani, harusi kucheza
Ni nusu ya dini, muloitimiza
In shaa Allah manani, awape mwangaza
Maarusi wetu, tunawapongeza
Na pia wazazi, pande zote mbili
Twawapa pongezi, kulitenda hili
In shaa Allah mwenyezi,awape sahali
Maarusi wetu, tunawapongeza
Mawadda na rahma, awape manani
Ndoani daima, muwe furahani
Muishi kwa wema, bila tafrani
Maarusi wetu, tunawapongeza
Muite vizuri, mwenza afurahi
Majina mazuri, si ya ikirahi
Izidi sururi, kumuita ruhi
Maarusi wetu, tunawapongeza
Walo wema wana, walosuluhia
Mola subuhana, kuwajaalia
Ya kusikizana, iwe familia
Maarusi wetu, tunawapongeza
It is not a poem ? I think it is because you have choice and stringing words with wonderful