
MAHITAJI YA SAMAKI
- Samaki mmoja mkubwa aliyesafishwa vizuri na kupigwa mitai(kukatwa mistari ili viungo viingie vizuri)
- kituKitu thomu kijiko 2 cha mezani
- Pilipili manga iliyosagwa kijiko 1 cha mezani
- Fish masala kijiko 1 cha mezani
- Ndimu/limau 1
- Chumvi kiasi
- Mafuta uto ya kumpaka samaki
MAHITAJI YA TUI
- Tui zito vikombe 3
- Currypowder kijiko 1 cha mezani
- Pilipili manga iliosagwa kijiko 1 cha mezani
- Mdalasini iliosagwa kijiko 1 cha mezani
- Kitunguu thomu kijiko 1 cha mezani
- Chumvi kiasi
MATAYARISHO
- Changanya viuongo vyote vya samaki kisha umpake samaki viungo hivi
- Mpake samaki mafuta uto kidogo juu ili asishike kwenye chuma wakati wa kumchoma(mpake Kwa tahadhari ili viungo visitoke)
- Mueke samaki kwenye chuma na umchome kwenye makaa. Akishaiva upande mmoja utamgeuza upande wa pili taratibu ili pia aive
- Samaki akienda kuiva, endelea na matayarisho ya tui
- Bandika tui motoni na ueke viungo vyote vya tui
- Koroga tui lako mpaka liwe zito Kwa takriban dakika 20(hakikisha tui ni zito Sana ili lishikane na kuwa zito haraka)
- Epua tui lako tayari kumpaka samaki
- Unaweza ukampaka samaki pale pale kwenye chuma ulomchomea au ukamueka kwenye chuma cha chapati umpake Kwa urahisi
- Anza kumpaka samaki wako upande mmoja kisha umgeuze umpake na upande wa pili
- Samaki Yuko tayari
- Andaa mezani Kwa mkate wa mofa
MAELEZO YA ZIADA
- Unaweza ukamchoma samaki Kwa oven pia. Utamueka kwenye chuma cha oven kisha chini ueke tray ili oven lisimwagikiwe na viungo likachafuka.
KWA MAPISHI ZAIDI UTANIPATA
- Instagram@farwats_kitchen
- Facebook@farwat’s kitchen
- You tube@farwat’s kitchen