
MAHITAJI YA ROJO
- Nyama nusu kilo(1/2 kg)
- Kitunguu thomu kilichosagwa pamoja na tangawizi kijiko cha mezani 1
- Pilipili manga iliosagwa kijiko cha mezani 1
- Bizari nyembamba/jira iliosagwa kijiko cha mezani 1
- Mdalasini iliosagwa kijiko cha mezani 1
- Maziwa mala vijiko vya mezani 5
- Pilipili boga 1 ilioiliokatwa katwa
- Vitunguu maji 3 vilivyokatwa katwa slices
- Nyanya 8 zilizoblendiwa(unaweza ukaziblend na carrots ukipenda)
- Tomato ya mkebe/paste vijiko vya mezani 4
- Dania 1
- Viazi 4 vikubwa vilivyokatwa katwa size ta kiasi
- Rangi ya viazi
- Mafuta ya kupikia/uto kiasi
- Chumvi kiasi
MAHITAJI YA WALI
- Mchele nusu kilo (1/2 kg)
- Mafuta ya uto vijiko vya mezani 3
- Rangi ya golden yellow na green
MATAYARISHO
- Weka nyama kwenye sufuria pamoja na mahitaji yote ya rojo isipokuwa viazi, rangi ya viazi, Kitunguu maji, dania na mafuta
- Koroga vizuri, ubandike motoni uache nyama iendelee kuiva(unaweza ukatumia pressure cooker ndio nyama iive haraka na ilainike vizuri)
- Kaanga Kitunguu maji mpaka kiwe golden brown kisha kiweke pembeni
- Weka rangi ya viazi kidogo na chumvi kwenye viazi na uvichanganye vizuri
- Vikaange viazi kwenye mafuta mpaka viive lakini visiive sana kisha viweke pembeni
- Tizama rojo lako na kama nyama imeiva na limekauka, weka viazi na vitunguu ulivyovikaanga, dania na mafuta uto na uliache lichemke Kwa dakika 5
- Rojo lipo tayari
- Endelea na matayarisho ya wali
- Bandika motoni mchele uliouosha vizuri na kuuroweka Kwa dakika kadhaa na ufunike mpaka uanze kuiva kisha mwaga maji
- Urudishe motoni na utie mafuta
- Tengeza shimo upande mmoja utie rangi ya golden brown na upande mwingine utie rangi ya green
- Funika wali wako uendelee kukauka na kuiva vizuri
- Biriani lipo tayari
- Andaa mezani Kwa kachumbari, pilipili ya kukaanga na juisi ya passion
KWA MAPISHI ZAIDI UTANIPATA
- Instagram@farwats_kitchen
- Facebook@farwat’s kitchen
- You tube @farwat’s kitchen
Shukran Jazakallahu kheir sister.
Nimependa sana mapishi yako.Allah akuzidishie.
Nimefurahi kuskia hivyo siz
Aaamiin