
‘Likuja mume tajiri, tena mweupe pepepe
Mama kaona fahari, akanioza peupe
Hakuchunguzwa vizuri, kumbe mume ni mapepe
Mengine yote bonasi, mume dini na tabia
Hata awe na majumba, na pesa mpwito mpwito
Ila kidini ayumba, na tabia ni nzito
Huyo si mume ni mamba, ‘takuachia majuto
Mengine yote bonasi, mume dini tabia
Au hizo siksi paksi, na sura ilo jamali
Lakini hayo maasi, afanya bila kujali
Huyo si mume ni nuksi, dadangu tia akili
Mengine yote bonasi, mume dini na tabia
Mtume wetu hashima, ‘metwambia umma wake
kuwa mume alo mwema, ni mwema kwa wake zake
Hivyo basi hima hima, kaka mutanabahike
Mengine yote bonasi, mume dini na tabia
Atapowajia kwenu, mume dini na tabia
Mwozeni mwari wenu, mtume ametwambia
itakuwa bora kwenu, kwani ndiyo sawa ndia
Mengine yote bonasi, mume dini na tabia
Mume dini tabia
Yafunza✓✓
Asante😊