
Podini(caramel pudding) ni aina ya kitindamlo maarufu sana pwani na duniani kote Kwa ujumla. Vile vile ni chakula kitamu sana na kinachopikwa Kwa mahitaji machache na ya kawaida.
MAHITAJI
🔸Mayai 6
🔸Sukari vijiko vya kula 6(ya caramel)
🔸 Sukari vijiko vya kula 6(ya pudding)
🔸 Maziwa nusu lita(500ml)
🔸iliki kijiko cha kula 1/2
🔸Ice cream flavour/vanilla (sio lazima)
MATAYARISHO
🔸Chemsha maziwa pamoja na iliki uyaache yapoe.
🔸weka sukari vijiko 6 kwenye sufuria uikoroge Kwa Moto mdogo mdogo mpka iyeyuke(usiweke maji) kisha iache ndani ya sufuria ipoe.(hii ndio inaitwa caramel)
🔸weka mayai, sukari Ile vijiko 6 ambavyo hatujavitumia, maziwa na vanilla/ice cream flavour kisha blend.(hii ndiyo pudding)
🔸mimina mchanganyiko ulioblend kwenye ile sukari ulioiyeyusha(caramel).
🔸Funika aluminium foil na ubake Kwa oven Kwa saa moja Kwa Moto 200°C mpaka ishikane na kuiva. Hakikisha tray ya oven umeweka maji.
🔸itoe kwenye oven na utoe aluminium foil. Weka sahani juu ya sufuria na ugeuze sufuria ili podini iingie ndani ya sufuria.
🔸weka Kwa fridge na userve ikiwa baridi.
MAZINGATIO
🔸Oven ziko tofauti, Kwa hiyo huenda podini yako ikachukua muda mchache au muda mwingi zaidi kuiva.Hivyo basi, kila baada ya muda, itazame podini yako kama ishashikana.
🔸Unaweza ukatumia jiko la makaa.weka maji kwenye sufuria kubwa kisha weka sufuria yako ya podini ndani na ufunike juu Kwa kitu kizito.
Kwa mapishi zaidi utanipata you tube@farwat’s kitchen.
Instagram@farwats_kitchen
Facebook@farwat’s kitchen
🌹🌹🌹